Shirika la Reli Tanzania – TRC limeendelea na zoezi la malipo ya fidia kwa wanachi waliotwaliwa maeneo yao kupisha mradi wa ujenzi wa reli ya kisasa mkoani Shinyanga na Mwanza, hivi karibuni Juni 2022.
Shirika la Reli Tanzania - TRC limetoa ufafanuzi juu ya ununuzi wa injini na behewa za abiria na mizigo kwa matumizi ya reli ya kisasa - SGR kwenye mkutano wa waandishi wa habari uliofanyika katika ukumbi wa mikutano TRC jijini Dar es Salaam Juni 15, 2022.