Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Shirika la Reli Tanzania

KIPANDE CHA PILI MOROGORO-MAKUTOPORA UJENZI WA SGR WAZIDI KUNOGA.


news title here
24
October
2019

Naibu Waziri wa Ujenzi Mhandisi Elias John Kwandikwa amezindua utandikaji wa Reli ya kisasa kipande cha Pili Morogoro - Makutopora hivi karibuni Oktoba 2019.

Katika hafla hiyo Naibu Waziri alimtaka mkandarasi aongeze kasi ili kuweza kumaliza kwa wakati.Aliongeza wakati wa uzinduzi wa zoezi la utandikaji reli katika eneo la Mkata mkoani Morogoro, Naibu Waziri Kwandikwa amesema kuwa, pamoja na kasi kubwa ya ujenzi wa Reli hiyo, lakini watanzania wamefaidika na fursa za Ajira za moja kwa moja zaidi ya elfu nne na viwanda vilivyopo nchini kuweza kuongeza mapato kama viwanda vya Saruji na Nondo kea kupata fursa ya kuuzia wakandarasi

Naibu Waziri Kwandikwa ameongeza kuwa, ujenzi wa Reli ya kisasa unaotekelezwa na Serikali ya awamu ya tano una lengo la kuboresha miundombinu ya reli na kuongeza ufanisi katika utoaji huduma za usafiri wa reli nchini na nchi jirani.

Katika gafla hiyo naye, Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania (TRC) Ndugu Masanja Kungu Kadogosa amesema kuwa, asilimia 90 ya eneo linalohitajika kwa ajili ya ujenzi wa Reli hiyo kipande cha Morogoro - Makutopora limekabidhiwa kwa Mkandarasi kampuni ya Yapi Markezi na kinachoendelea ni utekelezaji ili wamalize kwa wakati.

Sambamba na hafla ya utandikaji wa Reli kwa kipande cha pili Morogoro-Makutipora Naibu Waziri Kwandikwa akiongozwa na mwenyeji wake Mkurugenzi mkuu TRC Ndugu Masanja amepata fursa ya kutembelea eneo linapojengwa handaki refu zaidi kwenye ujenzi huo, lenye urefu wa Kilomita 1.4.

Kipande cha Pili ya ujenzi wa Reli ya kisasa (SGR) kipande cha Morogoro - Makutopora,Kinaendelea vema na tayari Serikali itagaramia kiasi cha shilingi Trilioni 4.7 kwa ajili ya utelekeza wa ujenzi wa SGR.